Category: sms
LAZIMA UCHEKE KINGEREZA CHA SHILOLE ”FAT WOMAN SHISHI” AWAVUNJA MBAVU WATANGAZAJI
ROSA REE AMKATAA FRIDA AMANI LIVE ”SIWEZI KUCHANA”
FRIDA AMANI: SINA MAZOEA NA SALAMA JABIR ”NI MKUBWA SANA”
Hizi ndo Jezi mpya za Taifa stars Zitakazotumika AFCON 2019
Vichekesho vya Mchaga Kwenye Kisima
Hebu fuatilia kichekesho hiki na angalia usivunjike mbavu
Kuna Mchaga mmoja kanasa kwenye kisima asubuhi na mapema akiwahi kibaruani. Kisima hicho kilitelekezwa na jirani yake
Baada ya maangaiko makubwa ya kumtoa, mmojawapo wa watoto wake alikuja na kamba na kumtupia ili waweze kumnasua kisimani.
Mahojiano yalikuwa hivi
Mtoto: Baba ebu daka hiyo kamba uing’ang’anie ili tukuvute mpaka utoke uko
Baba wa kichaga: Kwani hiyo kamba umenunua shilingi ngapi na kwa nani?
Mtoto: Nimenunua Shilingi elfu moja kwenye lile duka la mpare
Baba wa Kichaga: Alipatwa na mshangao haraka akajibu, Eyowii!! Amekuuzia ghali sana kijana, ebu rudisha na ukanunue kamba kwa Mosha anauza mia tano.
Wote: Wakashangaa, wakacheka na kuvunjika mbavu!
Vichekesho Mkutano wa Mandela na Nyerere Kule Ng’ambo ya Pili
Nyerere: Kama vile nakufananisha?
Mandela: Hata mimi naona sio sura ngeni?
Nyerere: We ndie Mandela eee?!
Mandela: Ndiyo mimi haswa miaka 14 ni mingi.
Nyerere: Sana!!.
Mandela: Sasa nitakaa wapi mbona hakueleweki huku?
Nyerere: We ngoja utapaelewa tu.
Nyerere: Eeh!! vipi huko Tanzania? ulitembelea hata hivi karibuni?
Mandela:
Eeeh! we acha tu, huko mara Zitto msaliti, mara Umeme mgawo miezi sita, mara mgomo wa Gesi haitoki Mtwara, mara kifo cha Mwangosi, mara Dawa za Kulevya, mara Meno ya Tembo, mara kuchoma Makanisa, mara mabomu kwenye mikutano ya hadhara na makanisani, mara Ufisadi, mara Dr. Ulimboka na Kibanda kung’olewa kucha na meno kwa plauzi, mara Division 5, mara Udini, mara ngumi Bungeni, mara kifo cha Dr Mvungi, mara tindikali kwa mapadri, mashehe na wageni, mara Kagame kuishambulia Tanznia, Petroli kuchakachuliwa, mara wengine wanasema eti Muungano ulioasisi unatokana na Visiwa vya Zimbabwe na Zanzibar na sio Tanganyika tena, mara muungano wa serikali tatu ndio unaotakiwa, mara Kigamboni kapewa Obama, mara Bushi na mke wake kaja Tanzania, Clinton na mke wake kaja Tanzania, Kamerun na mke wake kaja Tanzania, Xiing wa uchina kaja Tanzania, mara puttin wa Urusi kaja Tanzania. Yaani hekaya ni ndefu bora urudi ukayashuhudie mwenyewe.







